Search This Blog

Sunday 3 December 2023

 Semina kwa vijana katoliki kigango cha Kinyanambo c

DEC

17



SEHEMU YA I

(Kijana wa parokia ya mjini uko wapi)?

“FANYA MAAMUZI”.

Tuna mshukuru Mungu kutulinda kwa kipindi chote cha mwaka huu unaomalizika sasa.

Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya Kiongozi wetu Baba mt. aliyetutangazia mwaka wa huruma ya

Mungu naamini kila mmoja wetu amefaidika kwa kipindi hiki pekee. MAISHA YA HURUMA NA

MSAMAHA NDIO MAISHA YA MKRISTU hasa Mkatoliki.

MADA ZETU


1. KIJANA KATIKA HALI YA KUJITAMBUA

2. KIJANA NA MAISHA YA SAKRAMENTI

3. KIJA NA MAHUSIANO.

4. VIDEO (kama miundo mbinu inaruhusu)

1. KIJANA KATIKA HALI YA KUJITAMBUA

Somo WAEFESO 5:1-18. (Kuishi katika Kristo) TAFAKARI FUPI …………………………………………


 Maisha mapya ya kijana

 Kuishi kama watu wa Mungu na maisha ya kumpendeza Mungu. (Waefeso.5:3)

 Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu (pia kwa fedha na mali!!) Waefeso 5:6

(ni kwa nini sisi vijana hasa wakatoliki mnakuwa rahisi sana

kudanganyika)?.....................abuja declaration 1989…..effects on africa and the world. SALA

ZA NGUVU NA SALA-maamuzi.


 Sasa amka wewe uliye lala, na ufufuke kutoka wafu nae Kristo atakuangaza.

Kijana unaamshwa usingizini leo. Kipindi hiki cha Kanisa cha majilio je umejiandaaje? Umejipangaje?

MAANA YA MAJILIO KWA UFUPI

Majilio (pia: Adventi) ni kipindi cha liturujia ya madhehebu mbalimbali ya Ukristo (kama vile Kanisa

Katoliki, ya Waorthodoksi, Waanglikana na Walutheri) kinatangulia sherehe ya Noeli na kuanza

mwaka wa liturujia. Kinaweza kudumu kati ya siku 22 na 40.



Jina lake kwa Kilatini ni adventus maana yake ujio (wa Yesu Kristo), lakini jina la Kiswahili ni sahihi

zaidi kwa sababu linadokeza kuwa ujio wa Yesu ni kwa ajili yetu na kuwa alikuja zamani, anakuja kila

siku na atakuja kwa utukufu mwisho wa dunia.

KWA NINI KUWEPO NA MAJILIO ?

Sisi binadamu hatuwezi kuishi daima katika hali ileile bila ya matazamio. Hasa kijana anatarajia

mambo mapya tena mema. Hivyo tunajitahidi kuyapata. Asiyetazamia chochote amevunjika moyo,

hana hamu ya kuishi. Lakini matazamio ya kibinadamu yakimfikia mtu hayamridhishi moja kwa

moja. Kristo tu anatimiza hamu zote kwa kumkomboa kutoka unyonge.

Majilio yanatukumbusha kila mwaka matarajio ya kweli na hivyo yanaamsha hamu ya kuishi kwa

bidii ya kiroho.


MWAKA 2016 UMEFANYA NINI?

Huu ni mwezi wa 12/2016. Tangu January . tunamaliza mwaka sasa. wewe kama kijana mkatoliki

umeweza kufanya nini?

a. Kwa maendeleo yako ya kimaisha?. Je nimetimiza ya yangu ya msingi?( ya lazima? Hapa

kuna mambo MATATU tuwe makini.

I. Kuna mambo ya msingi YA LAZIMA. MF Elimu, ujuzi, kumjenga kujijenga

II. KUNA MAMBO MUHIMU( SI YA LAZIMA) mf.kuwa na simu, kusomea lugha nyingi,

kuwa na gari, kuoa na kuolewa,

III. KUNA MAMBO YA KIFAHARI (SI YA LAZIMA) mf. Kuwa na nyumba nzuri, vitu vya bei

ya juu; cm ya bei ya juu….na mambo kama hayo…

b. Kwa faida ya wale wanaokuzunguka? Mfano familia yako

c. Kwa bidii katika kukua kiroho? Je umeachia tu mwaka huu upite? (Pigamaesabu)

 Umewekaje mahusiano yako kipindi chote cha mwaka huu wewe na Mungu wako?

Umeweza kufanya yale ya msingi anayotaka Mungu au umejifanyia ya kwako?

 Ni vizuri sasa kjiweka tayari kwa mwaka ujao usijekuwa mwaka wa majuto na

masononeko.

 Matarajio yako yamekamilika au ulikata tama?

 Ni vema kujiuliza ndio mtu uweze kupiga hatua inayofuata.

 Waefeso6:1ff “enyi watoto watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema. Je

nimeyatenda hayo? Nimewaheshimu wenzangu?, nimewajali wenzangu?

Nimesababisha madhara kwa mwenzangu kiasi gani? Je nimeoomba msamaha?

d. Nijiwekee malengo mwa 2017.

 Mshirikishe Mungu katika maisha yako. (Jermiah 33:3) “niite nami nitakujibu na

kukuambia mambo makubwa yaliofichika ambayo hujapata kuyajua”.

 Munguhatakufanya udhauliwe tena (YOEL 2:19b)

3

Fr Haki semina ya vijana Dec.10/12/2016

Maswali kama yapo……………….

SEHEMU YA II

2. KIJANA NA SAKRAMENTI YA KITUBIO

Mara nyingi sakramen ya Kitubio ndio huwa inachangamoto nyingi sana na kwamba watu wengi

hawaipokei. (jiulize mara mwisho ulipo ipokea je ilkuwa kwa usahihi wake?

Sakramenti ni miferji ya neema kwa hiyo ni lazima ziwe na changamoto.

Tuangalie changamoto hizi kwa miwani ya kijana wa leo. Kijana anatatizo kubwa kuielewa na kuithamni

sakramenti hii ya upatanisho. Tutaje tu baadhi ya vikwazo;

 Kijana wa leo hana imani kuwa Mungu kweli anaweza kumsamehe dhambi. Ni wasi wasi ambao

unajengwa na jinsi anavyorudiarudia kuanguka katika katika dhambi. Ila Kristu alitufundisha

kusamehe mara ngapi? Je wewe ulishawahi kumkosea Mungu mara mia nne na sabini? Usikate

tama “Tukikumbushe “Haya njooni tusemezane, asema Bwana, dhambi zenu zijaapokuwa

nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera zitakkuwa

kama sufu” (Isaya.1:18).

 Kijana wa leo haoni umuhimu wa Sakramenti ya wongofu. Tatizo ni nini? Labda haoni tatizo. Je

unaweza kula chakula bila kunawa mikono?.....kadiri unavyojitahidi kimwili kuwa safi basi pia

tunahitaji kuwa safi KIROHO. AU wataka upate kipindupindu cha kiroho?

 Kijana wa leo anaishi kwa HOFU. Nikienda kuungama Padri atanijua kuwa mimi ni mdhambi.

Tena ni kujidhalilisha watu wakiniona nikisubiri zamu yangu….kwanini tunaanza kuwa na hofu

baada ya kutenda dhambi? Hofu ya kweli ingetushtua na kuacha kutenda dhambi. Kujidhalilisha

ingekuwa ni pale tunapoanguka dhambini….iweje isiwe kujidhalilisha unaposubiri kuingia

kwenye danguro wamsubiri mwenzako na iwe unaposubiri kuungama?..kama upo hodari wa

kutenda dhambi , yakupasa kuwa shujaa wa kuungama.

 Kijana wa leo analalamika sana. Kwa familia zetu neno msamaha ni nadra sana. Kosa likitokea

anatukanwa,kupigwa…kafundishwa kusamehe…tujilelee ktka mazingira ya kusamehe ndio

zawadi kubwa tunawezotoa.

 Kijana wa leo anaogopa kuungama kwa hofu ya kuchemsha. Hakumbuki tena namna ya

kuungama.

 Kijana wa lwo anazungukukwa na watu wa imani mbalimbali anasoma vitabu na magazeti

yenye mitazamo tofauti. Usimwige mwenzako….!!!

 Kijana wa leo anayumbishwa na mtazamo wa jamii. Neno “dhambi” katika jamii halina tena

maana. Limepitwa na wakti. Kosa kuwa kosa siku hizi ni mpaka ukamatwe. Jiunge kwenye vyama

vya kitume usifikiri wao ni wadhambi zaidii….

 Kijana wa leo anazungukwa na utamaduni wa uovu. Jamii imehalalisha mengi,kila kitu ni ruksa

kama kinakupendeza….mengine yamepewa majina ili kufisha uhalisia..mf. TENDO LA NDOA

lilipewa jina hilo ili kuonesha nani hasa anastahili ila kwa sasa lina majina mengi kama uroda n.k

kuonesha ni jinsi gani tunapenda vitamu tamu!! Uongo unaitwa….soga, wizi unaitwa kusogeza,

daya ya kulevya inaitwa unga, rushwa inaitwa toa kitu kidgo, hayo ndio maisha ya leo,kutoa

mismba kunaitwa kusafisha, kushusha ingini n.k kijana anazongwa na mambo mengi sana ni

lazima kuwa makini sana. Kijana unakwenda na fasheni, unakwenda na wakati wakati gani?

Heri uende na wa kati wa kufa na kufufuka kuliko wakati wa kufa na kuoza.

 Baba nae anaitwa ‘dadi’ .Funguka kijana. (Mt. 9:2) “Jipe moyo mwanangu, umesamehewa

dhambi zako”


SEHEMU YA III

3. KIJANA NA MAHUSIANO.

Krismasi na sherehe zake huleta furaha sana kama umejiandaa vyema na wengi huishia katika kujuta

pia maana wanashereheka kupita kiasi.

Kijana ni lazima aweze kutofautisha mambo haya.

 Urafiki na uchumba……majina yanayotumika

 Uchumba- maisha ya uchumba

 Uchumba sugu-kuishi gizani, kwenye matope

Kijana ni lazimza aweze kujichaguliwa mwenza wake bila msukumo wowote na baada ya

maandalizi mazuri. (msibake ndoa)

Ni lazima kuwa na mawazo chanya kwa mwenzako na kutamani mwenzako afanikiwe kama

wewe.


Kuchagua mchumba hapa kuna kazi kwel kweli. Ila basi mpe Mungu nafasi katika kumchagua

mwenza wako usijeingia matatani. MZIKI MARRY ME….

Maisha ya kujaribu ndo inamadhara gani?

-mimba za utotoni

-Kutoa mimba

-Kutumia madawa (visibiti mimba) ambayo madhara yake mwayajua mnaotumia ni

makubwa sana.

Maswali kama yapo.


SEHEMU YA IV -FILM USINIUE.

 Maisha ya ndoa ni maisha matakatifu, ndoa iheshimiwe, isichezewe, ndoa ni

sakrmenti. Mungu ameiweka kwa malengo maalumu ya uumbaji na si

KUJIFRUHISHA.

MWISHO…..MUNGU AWABARIKI NYOTE NA MERRY XMASS.

Posted 12th December 2016 by NIC

 

0 Add a comment

Loading


Sunday 8 May 2022

moja ya askari polisi warembo

Utawezana! Picha Matata za Makarau 6 Utakaotamani Wakukamate <script async src="https://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js?client=ca-pub-7458430346762429"

     crossorigin="anonymous"></script> Wowote

kiswahili.tuko.co.ke
May 6, 2022 9:08 PM

Hii ndio orodha ya maafisa wa polisi wa kike wanaoongoza kwa kuwa warembo zaidi. Urembo wao huwafanya wanaume kugeuza vichwa vyao kuwaangalia na baadhi hutania kwa kusema, wao hutamani kukamatwa na maafisa hao warembo.

TUKO.co.ke imefanikiwa kukupa ufafanuzi mdogo kuwahusu na kumbuka orodha hii haijapangwa kulingana na ni nani mrembo kuliko mwingine.

1. Serah Mwongeli

Picha safi za maafisa wa polisi 6 wa kike wanaoongoza kwa urembo, wanatikisa anga Kenya
Mwongeli aka Sessy, ni mzawa wa Mombasa na awali alikuwa mwalimu wa shule ya upili kabla ya kujiunga na jeshi la polisi. Picha: UGC Chanzo: UGC

Pia Soma: Waigizaji 10 mastaa wa kike wa asili ya Afrika wanaotikisa anga ya filamu Hollywood

Yeye ni afisa wa polisi wa Utawala katika Chuo cha Mafunzo ya Polisi cha Utawala huko Embakasi, Nairobi. Mwongeli aka Sessy, ni mzawa wa Mombasa na awali alikuwa mwalimu wa shule ya upili kabla ya kujiunga na jeshi la polisi. Kwa sasa anakaribia kukamilisha masomo ya Sheria katika Chuo Kikuu cha Nairobi.

2. Alice

Picha safi za maafisa wa polisi 6 wa kike wanaoongoza kwa urembo, wanatikisa anga Kenya
Yeye ni mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Mount Kenya ambapo anasomea jinsi ya kukabiliana na Uhalifu (Criminology). Picha: UGC Chanzo: UGC

Almaarufu The Baby Police alizaliwa na kukulia eneo kubwa la Mlima Kenya. Yeye ni mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Mount Kenya ambapo anasomea jinsi ya kukabiliana na Uhalifu (Criminology). Hivi sasa anatoa huduma zake huko Mumias, Kaunti ya Kakamega.

3. Josephine Wambui

Picha safi za maafisa wa polisi 6 wa kike wanaoongoza kwa urembo, wanatikisa anga Kenya
Alilelewa katika eneo la Limuru, Kiambu. Anafanyia kazi katika Kituo cha Polisi cha Kilimani jijini Nairobi. Picha: UGC Chanzo: UGC

Kwa jina lingine ni J Riva. Alilelewa katika eneo la Limuru, Kiambu. Anafanyia kazi katika Kituo cha Polisi cha Kilimani jijini Nairobi. Yeye ni kifungua mimba na kwa sasa anasomea Uhusiano wa Umma na Diplomasia.

J Riva anapenda masula ya urembo na fasheni ni moja ya vitu vinavyomfanya kuwa maarufu hasa unapochungulia picha zake mitandaoni.

4. Patricia Mwarashu

Picha safi za maafisa wa polisi 6 wa kike wanaoongoza kwa urembo, wanatikisa anga Kenya
Mwarashu pia anaitwa Tricia. Alizaliwa na kukulia katika Kaunti ya Mombasa. Picha: UGC Chanzo: UGC

Mwarashu pia anaitwa Tricia. Alizaliwa na kukulia katika Kaunti ya Mombasa. Hivi sasa yuko katika Kaunti ya Machakos anakofanyia kazi. Katika familia yao wapo wawili tu.

5. Rehema Swaleh

Picha safi za maafisa wa polisi 6 wa kike wanaoongoza kwa urembo, wanatikisa anga Kenya
Jina lake la utani ni Ella Chloe. Picha: UGC Chanzo: UGC

Jina lake la utani ni Ella Chloe. Yeye ni binti wa Kiislamu, alizaliwa na kukulia katika Kaunti ya Kisumu. Anafanya kazi katika Kituo cha Polisi cha West Park huko Lang'ata, Kaunti ya Nairobi.

6. Linda Okello

Picha safi za maafisa wa polisi 6 wa kike wanaoongoza kwa urembo, wanatikisa anga Kenya
Aligonga vichwa vya habari miaka kadhaa nyuma baada ya picha yake akiwa amevalia kimini iliposambaa kwa kasi mitandaoni. Picha: UGC Chanzo: UGC

Hatuwezi kufunga shughuli hii bila ya kumuorodhesha na kumtaja Linda.

Aligonga vichwa vya habari miaka kadhaa nyuma baada ya picha yake akiwa amevalia kimini iliposambaa kwa kasi mitandaoni. Badala ya sketi ya kawaida, Linda alikuwa ameifanya kuwa fupi na iliyobana sana makalioni.

Wajibu wake ulikuwa afisa wa trafiki na alifotolewa akiwa kazini kando ya barabara ya Kiambu-Ruiru.

Baadaye hatua za kinidhamu zilichukuliwa dhidi yake na aliteremshwa cheo kutoka Idara ya Trafiki na kupelekwa Molo kuwa afisa wa majukumu jumla.

Mwandishi ni Ali Hassan Kauleni, Kaunti ya Nairobi

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.


Tuesday 22 March 2022

maisha ng'ombe ahukumiwa maisha


Mlisha ng’ombe afungwa maisha kwa kulawiti mtoto wa miaka saba

TUESDAY MARCH 22 2022
mauajipic
By Mary Sanyiwa

Mufindi. Mahakama ya Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa, imemhukumu mkazi wa Kijiji cha Kitelewasi, Godi Waya (30) kifungo cha maisha baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumlawiti mtoto wa miaka saba (jina linahifadhiwa).

Godi ambaye aliajiriwa kulisha ng’ombe wa bibi wa mtoto huyo alidaiwa kumtoa mwathirika chumbani kwake na kumpeleka chumba anacholala na kuanza kumbaka huku akiwa amemziba mdomo na kumtisha asimwambie mtu alichofanyiwa.

Hakimu Mkazi Edward Uphoro alikataa utetezi wa mshtakiwa huyo kuwa alibambikiwa kesi hiyo. Amesema kulikuwa na ushahidi wa kutosha kuwa yeye ndiye aliyefanya kitendo hicho na mwathirika alionekana akitoka chumbani kwake akiwa uchi.

“Suala la kubambikiwa kesi halina mashiko kwa sababu kuna ushahidi wa kimazingira na mshtakiwa mwenyewe alikiri mahakamani kuwa mtoto huyo alitoka chumani na kwamba alikuwa na mazoea ya kuingia chumani kwake. Swali ni je, kwa nini alitoka akiwa uchi?  

“Mahakama hii imejiridhisha kuwa ushahidi uliotolewa na mwathirika pamoja na bibi yake ulikuwa na uzito wa kumtia mtuhumiwa hatiani kwa kosa la kulawiti,” amesema

Hakimu huyo amesema mahakama inatoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine wenye matamanio kama hayo kwani vitendo hivyo vimekithiri katika jamii na kusababisha watoto kuishi kwa wasiwasi katika mazingira yanayowazunguka.

ADVERTISEMENT

"Vitendo hivi vimekuwa vikisababisha watoto kuharibika na kuwa mashoga, hivyo, mahakama hii inatoa adhabu kali ya kifungo cha maisha kwa Godi Waya ili iwe fundisho kwa jamii kuhusu vitendo hivi," amesema.

ADVERTISEMENT

Friday 18 March 2022

urusi yaionya Marekani

Urusi yaonya Marekani: Tutawararua na kuwaweka katika nafasi yenu, msitujaribu!

kiswahili.tuko.co.ke
Mar 18, 2022 11:55 AM
  • Urusi imeonya Marekani kuwa ina uwezo wa kuirarua Marekani kwa vipande na kuiweka katika nafasi yake
  • Urusi inaituhumu Marekani kwa kuendeleza njama ya kuisambaratisha kwa kuchochea ulimwengu dhidi yake, utawala wa Moscow ukisema hilo halitawezekana
  • Onyo la Urusi linajiri siku mbili tu baada ya taifa hilo kumpiga marufuku Rais wa Marekani Joe Biden kukanyaga nchini humo

Urusi imeonya Marekani kuwa ina uwezo wa kuirarua Marekani kwa vipande na kuiweka katika nafasi yake, utawala wa Moscow ukiituhumu serikali ya Jose Biden kwa kuendeleza mipango ya kuisambaratisha Urusi.

Urusi Yaionya Marekani dhidi ya Kuendelea Kuichokoza: "Msitujaribu, Tutawararuararua kwa Vipande"
Rais wa Marekeni Joe Biden (kushoto) na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin.

Dmitry Medvedev ambaye alihudumu kama rais wa Urusi kati ya 2008 na 2012 na ambaye kwa sasa ni Katibu wa Baraza la Usalama la Urusi alisema kuwa Marekani ilikuwa na njama ya kuuchochea ulimwengu dhidi ya Urusi ili kushurutisha taifa hilo kupiga magoti.

“Haitafaulu. Urusi ina nguvu za kuwaeka maadui wetu katika eneo lao,” Medvedev alisema.

Tangu kuvamia Ukraine mnamo February 24, Marekani na maswahiba wake wa bara Ulaya na Asia, wamewaekea vikwazo viongozi wa Urusi, kampuni za Urusi, wanabiashara wa taifa hilo na kuitenga Urusi kwenye uchumi wa dunia.

Msitulaumu: Urusi Yasema Vikwazo vya Marekani Kulaumiwa kwa Gharama Kubwa ya Maisha Kenya

Rais Vladimir Putin anasema kuwa kile anachoita ‘oparesheni spesheli nchini Ukraine’ kilihitajika kwa sababu Marekani ilikuwa ikiitumia Ukraine kuitishia Urusi na Urusi haikuwa na budi ila kulinda raia wake dhidi ya kuangamizwa na Ukraine.

Onyo hili linajiri siku mbili tu baada ya taifa hilo kumpiga marufuku Rais wa Marekani Joe Biden kukanyaga nchini humo pamoja na aliyekuwa Katibu wa Serikali ya Marakeni Hillary Clinton pamoja

Dayamondi ashika nafasi ya tatu

Mjadala Waibuka Diamond Namba 3 Afrika, CNN Wamaliza Ubishi

globalpublishers.co.tz
Mar 17, 2022 8:30 AM

Mjadala mkubwa unaoendelea kwenye Social Networks hivi sasa, ni kuwa Diamond si miongoni mwa wasanii watatu wakubwa barani Afrika, Hizi research au mitazamo hufanywa na watu kulingana na namba na mafanikio ya msanii husika na sometimes kwa mwaka husika pia,ni kazi ya msanii mwenyewe kumantain.

Kwa Diamond inawezekana hasiwe na impact kubwa barani Afrika kote kwasababu moja kuu,ametengeneza utajiri mkubwa wa mashabiki ukanda wa Afrika Mashariki na kati, hawa watu wamempatia followers, subscribers na hata streams kwa kiasi kikubwa, kwahiyo ukimuweka kwenye mafanikio ya Namba,basi atapambana vizuri na wasanii wengine tunao waona wao ndio wanastahili kuwa wasanii wakubwa Afrika.

Kimafanikio, Diamond kafanikiwa kwa kiasi kikubwa sana, ni miongoni mwa wasanii watano bora wenye tuzo nyingi barani Afrika,muziki wake umeenda mbali zaidi,na amekuwa nominated/Winner kwenye tuzo kubwa duniani kama MTV EMA, BET, n.k, unaanzaje kumpuuza msanii huyu?

2019 CNN walimtaja Diamond kama msanii namba 3 kwa ukubwa barani Afrika, nyuma ya Burna Boy, na mwanamama Angelique Kidjo. Lakini pia ametajwa na vyanzo vingi kwenye top 3 ya wasanii wakubwa Barani Afrika.

Diamond ameibua mjadala huo alipokuwa akifanya mahojiano na Wasafi FM wakati wa kutambulisha EP yake mpya inayokimbiza kwa sasa kwenye platforms zote iitwayo FOA.

Tuesday 28 September 2021

Tutamkumbuka daima

Mazingira yetu tuyatunze: Tutamkumbuka daima:  Huyu ni rais John pombe magufuli alikuwa rais was Tanzania aliaga dunia tarehe 17 mach 2021 kwa ugonjwa wa moyo. Alichaguliwa mwaka 2015 Katika uchaguzi mkuu.Aliweza kuanzisha shughuli mbalimbali za maendeleo kama ujenzi wa barabara za juu ili kupunguza msongamano Katika barabara za Dar es saam.Aliwezesha uanzishaji wa maduka ya madini kila wilaya nchini.Aliwezesha uwajibikaji wa wafanyakazi.Alianzisha miradi mikubwa ya reli ya mwendokasi.Alianzisha bwawa kubwa la kufua umeme.Aliwawezesha wajasilia Mali kufanya kazi zao bila bugudha. Alituonesha kuwa sisi tunaweza.
Kwakweli tutamkumbuka daima.